HAKIKISHA UMEISOMA HII.
HAKUNA MTU ASIYEWEZA KUFANIKIWA KIUCHUMI AKIAMUA Siku kadhaa zilizopita nilikutana na hawa kina dada wawili mtaani (mitaa ya Sinza) wakiwa wamepumzika baada ya kazi kubwa ya kutembeza mboga za majani mtaani. Walikuwa wamechoka hakika na walikuwa wamekaa mahali dukani wakiwa wameagiza zao soda baridi kushushia kidogo na labda kulainisha koo kwa sababu ya kazi nzito ya kutembea juani na huku ukiita kwa sauti: "Haya jamani mchicha, mnafu, matembele, mchichaaaaa". Niliwasalimia na kukatisha safari yangu ili nikae nao pia ili niendelee kujifunza maisha ningali hapa duniani. Ama baada ya salamu na maneno mawili matatu ya "Breaking the Ice" nikaanza kureason nao mambo ya biashara na hasa biashara yao. Mimi: Hebu niambieni nyinyi changamoto yenu hasa ni nini kwenye hii biashara? Mmoja wao: Dah kakangu changamoto ni nyingi mno lakini kubwa ni kwamba watu siku hizi wanaogopa kula mboga za majani si unasikia sijui serikali wanasema mboga zisilimwe sehemu za maji yeny...